Pages

Wednesday, April 5, 2017

DENGU HUSAIDIA KUONGEZA NGUVU ZA UZAZI.



Dengu zao muhimu jamii ya mikunde linalolimwa na kutumiwa duniani kote, hasa nchi za kiafrika na kiasia.Jina la kibotania huitwa cicer arietinum l. Waingereza huita chickpea . Ni chanzo kizuri cha wanga na protini, na protini yake inachukuliwa kuwa ni bora kuliko ya mikunde mingine.  Dengu ina kiasi muhimu cha asidi ya amino za msingi kasoro asidi zilizo na salfa “sulphur“ ambazo zinaweza kukamilishwa kwa kuongeza nafaka katika mlo wa kila siku . Kwenye  kuna hifadhi ya wanga , ikifuatiwa na nyuzinyuzi za chakula, oligosaccharides na sukari rahisi kama vile glucose na sucrose. Ingawa kunapatikana kiasi kidogo cha mafuta ( lipids) Dengu ina utajiri wa asidi  za mafuta zisizodhuru muhimu kwa virutubisho kama vile linoleic na oleic acids. Kwenye punje za Dengu pia kunapatikana madini ya calcium , magnesium , phosphorus, chuma na K.
     Dengu ni chanzo kizuri cha vitamin muhimu kama vile riboflavian ( vit B2), niacin ( vit B3), thiamin ( vit B1), Folate na vitamin A (B-Carotene) kama ilivyo mikunde mingine Dengu ina sababu za kuondoa virutubisho visivyofaa ( anti – nutritional factors) kutokana na mbinu mbalimbali za mapishi Dengu zina faida kadhaa kiafya na muunganiko wake   na mikunde na nafaka nyingine unaweza kuwa na athari nzuri kwa magonjwa ya binadamu kama vile kisukari aina ya pili ( type 2 diabetes)  magonjwa  ya mmeng’enyo wa chakula, na baadhi ya saratani, kuondoa udhaifu wa mwili, uchovu na mengineyo, homa, magonjwa ya mfumo wa kupumua na kukojoa, abscesses, husaidia upungufu  wa damu mwilini, hurekebisha lehemu ( cholesterol) na mengineyo.
    Kwa wale wenye kusumbuliwa na matatizo ya nguvu za uzazi  na hawana matatizo ya mzunguko wa damu watumie mara kwa mara, mfumo wa neva , mfumo wa mkojo, homoni na kemikali na utendaji  wa viungo vingine ni vizuri wakatumia Dengu mara kwa mara.  Wananchi wa nchi za Asia kama India , China ,Japan , Indonesia na nyingine zinatumia sana Dengu, soya,  nk. Nchi hizi zina watu wengi duniani kuliko hata  ukubwa  wa  nchi zao.  Na utumiaji wa Dengu mara kwa mara kwa watu wenye kisukari hurekebisha kiwango cha sukari kwenye insulin.  Watanzania wote tuanze kutumia Dengu  mara kwa mara ili kuimarisha nguvu za uzazi kwani sasa hivi  vijana wengi wanalalamika kuwa hawana nguvu za uzazi .
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com
Blogu: mazingiranp.blogspot.com

3 comments: