Pages

Wednesday, April 5, 2017

MULIMULI HUTIBU TUMBO NA MAGONJWA YA ZINAA






Mulimuli ni mti unaokuwa na kufikia mita 10 hadi 15 kutokana na mazingira uliopo. Hupatikana sehemu nyingi Tanzania. Jina la kibotania hiutwa Cassia abbreviata. Waingereza huitwa Long-pod cassia, longtail cassia, sjambok pod. Kiswahili huitwa Mkakatika au mbaraka.
Wahehe huita Limulimuli, Wagogo huita mkakatika au mulimuli, wasukuma huita Nunda Lunda, wanyamwezi huita Mulunda lunda au munzoka, wasambaa huita mzangazi au msangani, wamwera huita mchenamela, wadigo huita muhumba mkulu, wataita huita msoko.
Mulimuli ni mti unaopendwa sana Africa mashariki kwa matumizi ya dawa kutibu magonjwa mbalimbali. Majani yakivutwa kama sigara hutibu Haematuria, mizizi au unga wa mizizi ikichemshwa na maji hutibu maumivu ya tumbo, kuuma meno unachukuchua, kichocho, matatizo ya gastrointestinal, kisonono, kaswende, Nimonia, matatizo ya uterus kwa wanawake, Hedhi iliyozidi(nzito) kwa wanawake, kuumwa na nyoka, kuongeza hamu ya tendo la ndoa, kuharisha, malaria, Homa, Homa ya Blackwater, minyoo, maumivu ya kifua na vichomi.
Majani yaliyochemshwa na mizizi hufaa kuoshea macho kwa kutibu Ophthalmia. Majani yake yakipondwa hutumika kuwakimbiza nyoka katika mapango yao.
Mulimuli ni rafiki wa mazingira na pia hutumika kutengenezea samani, mitwangio na nguzo za kujengea nyumba n.k.

Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com
Blogu: mazingiranp.blogspot.com

1 comment:

  1. Asante sana kwa kutufunza faida nyingi kwa huu mti ningependa kujuwa jee nikiuhitaji wa unga nitaupataje?

    ReplyDelete