Pages

Wednesday, April 5, 2017

EMBE HUREKEBISHA KIWANGO CHA INSULINI MWILINI


Mwembe hustawi katika maeneo ya joto na nyanda za chini. Mti unafikia urefu wa meta 25, huota maeneo yote ya tropiki. Jina la kibotania huitwa mangifera indica, na waingereza huita mango, wandali na wanyakyusa  huita  umwembe. Maembe  hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Tabora, Pwani, Mtwara, Tanga, Mwanza, Morogoro na Mbeya. Maembe ni zao muhimu la biashara na chakula. Sehemu zinazotumika ni, Majani Machanga, matunda, kokwa (mbegu), magome (gamba), maua, mizizi nk.  Ili kuyalinda maisha ya mti, chukua magamba kutoka kwenye matawi tu (na iwe kutoka upande mmoja tu)
Tunda hili, licha ya ladha yake nzuri pamoja na utamu wake, linaweza kutumika kwenye milo yote kwa siku kwenye familia nzima.
Ulaji wa mara kwa mara wa tunda hilo husaidia kupunguza kiwango cha asidi mwilini, kuboresha mmeng’enyo wa chakula na kurekebisha kiwango cha insulini. Husaidia kusafisha damu pia, kuimarisha muonekano wa ngozi, kuzuia saratani na kuimarisha kinga ya mwili. Hupunguza mawe kwenye figo. Faida nyingine ni kuongeza madini ya chuma kwa wajawazito, kupunguza uzito na kulinda macho dhidi ya magonjwa.
Unywa wa juisi yake kila siku husaidia kuleta uoni mzuri kwa sababu juisi hiyo ina vitamin A ambayo huimarisha afya ya macho na kuwasaidia wale wenye macho makavu au wasioona vizuri hasa usiku.
Hata hivyo,juisi ya embe inapotumika bila kuweka sukari ni nzuri kwa watu wenye kisukari kwa sababu husaidia kurekebisha tatizo hilo pamoja na kurekebisha mapigo yamoya kuwa sawa na kuondoa sumu mwilini.
Vilevile juisi hii inasifika kwa kuimarisha mmeng’enyo wa chakula na huondoa ukosefu wa choo ikichanganywa na nanasi.
Licha ya vitamin A, juisi ya embe ina vitamin C pamoja na carotenoids ambazo husaidia kurekebisha kinga za mwili hivyo kuwafaa zaidi wenye upungufu wa kinga hizo, wanaonyemelewa na magonjwa au wenye maradhi ya muda mrefu mfano pumu.
Embe linafaida kubwa katika afya ya ngozi kwani ukipaka maganda ya embe usoni na kukaa nayo kwa muda usiopungua dakika kumi kasha ukanawa kwa maji yanayotiririka au yale yanayotoka bombani husaidia kuifanya ionekane vizuri.
Majani machanga ya mwembe yakichemshwa hutibu kuharisha, kuharisha damu, kikohozi, pumu, matatizo ya kifua, homa, bawa siri (haemorrhoids) tumia majani makuukuu na chemsha katika lita 5 za maji kwa dakika 30, chuja na tumia mtokoso huu kwa kuoga sehemu za mapaja, kuoshea kinywa na maumivu ya fizi, kuoshea vidonda vya nje ya mwili, unga wa majani unafaa kwa kutunza meno kwa kusukutulia, maua hutibu minyoo. Tunda lake likiliwa hutibu kuvimba fizi, linaondoa makamasi kifuani kwenye mirija ya hewa, bandama lililotanuka unachanganya na asali kijiko cha chai, matatizo ya tumbo na ini unachanganya na maziwa fresh, vipele vya joto unachemsha maembe 2 mabichi na vikombe 2 vya maji ikipoa unachuja na kuongeza chumvi au sukari kwa ladha, unakunywa mara moja kwa siku, embe bichi vipande 6 vinaweza kuondoa mawe katika figo kwa wiki moja tu vikiliwa kila siku, pigo la moyo ni kuchemsha embe bichi, chumvi na sukari kunywa, ukiinusa sana juisi yake inasitisha utokaji wa damu puani (mhina), na juisi ya embe na maziwa ni kirejesho kizuri cha afya, Tumia mara kwa mara. Unga wa mbegu ukinywa mara 3 kutwa hutibu kuharisha na kuhara damu, uzazi wa majira tumia mbegu ya embe , mbegu ya embe hutumika kulegea kwa uzazi wa mwanamke, na utoaji wa maji meupe kwenye uke, (leucorrhea) . Gome (gamba) hutumika kutoka damu nyingi kuliko kawaida kwa mwanamke, vidonda vya kooni na homa.
Maembe husindikwa ili kupunguza upotevu, kuongeza thamani na matumizi ya zao. Embe husindikwa kupata bidhaa mbalimbali kama vile juisi, achali, chatine na maembe yaliyo kaushwa nk.
Athari, majani makuukuu yatumike kwa kusukutua tu.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com
Blogu: mazingiranp.blogspot.com

No comments:

Post a Comment