Pages

Wednesday, April 5, 2017

BEETROOT NI NZURI KWA WENYE MAWE KWENYE FIGO


Namshukuru mwenyezi mungu kwa kunipa afya njema kunifikisha 2017. Nilichojifunza ni kwamba watu wengi hawafahamu faida za vyakula tunavyo kula.
Watu wengi hawajui faida za beetroot na hii ndiyo sababu iliyonifanya niandike makala hii ili kuwaelimisha watu wengi. Asili ya Beetroot ni ulaya na imetumiwa na wagiriki na waroma kwa miaka mingi iliyopita. Jina la kibotania Beta vulgaris. Na sasa Beetroot  inalimwa ulimwenguni pote. Kinachotumiwa ni majani na mizizi.
Juisi ya Beetroot ni moja ya juisi bora kwa afya ya binadamu. Beetroot ni chanzo kikuu cha sukari ya asili, calcium, sodium, potassium, phosphorus, sulphur, chloline,iodine,chuma,shaba,choline, vitamin B1,B2, Niacin,B6 na C.
Juisi ya beetroot ni nzuri sana kwa Figo na gall bladder. Madini ya chuma yaliyomo kwenye beetroot yanafaa kurutubisha Anaemia. Juisi ya Beetroot ikichanganywa na karoti na Tango ni nzuri sana kwa wenye upungufu wa nguvu za kiume, mawe ya kwenye Figo,gall bladder, Ini, matatizo ya tezi dume (Prostate troubles) na kutengeneza damu mwilini. Beetroot ni kizuia saratani. Juisi ya beetroot ni nzuri kwa kichefuchefu na kutapika kuna tokana na tindikali (acidity), Homa ya manjano, hepatitis, kuharisha, kutosagika kwa chakula na Dysentery. Juisi hii ichanganywe na juisi ya ndimu ndio inakuwa bora zaidi. Juisi ya Beetroot ikichanganywa na kijiko cha Asali na ikanywewa asubuhi kabla ya kifungua kinywa ni nzuri kwa vidonda vya tumbo aina ya gastric ulcer. Juisi ya majani ya beetroot ikichanganywa na juisi ya ndimu ni nzuri kwa homa ya manjano na vidonda vya tumbo (gastric ulcer)kama inanywewa mara moja kila siku.
Ulaji wa kila siku wa Beetroot huzuia ugonjwa wa kukosa choo na piles.
Juisi ya Beetroot ikitumiwa mara kwa mara utaepukana na magonjwa ya hypertension, arteriosclerosis na matatizo ya moyo.
Wazungu na watu wa Asia hutumia Beetroot kama mboga, salad, juisi na supu.
Watanzania tuanze kutumia Beetroot kwa faida ya afya zetu.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com
Blogu: mazingiranp.blogspot.com

3 comments: