Pages

Wednesday, November 6, 2013

MAAJABU YA Gotu Kola



KUIMARISHA KUMBUKUMBU (IMPROVING MEMORY)
CENTELLA ASIATICA au Gotu Kola, Indian Pennywort, Marsh Penny ni mmea unaoota kwa kutambaa. Na huota sehemu zilizo na unyevu mwingi na kwenye kingo za mito. Mmea huu umekuwa ukitumika sana huko mashariki ya mbali India, China, Japan, Indonesia na nchi za Amerika. Hapa nchini Tanzania ni watu wachache sana wanaotumia, na hii inatokana na watu wengi kutoufahamu kazi yake japo wanauona wanapokuwa kwenye shughuli zao nyingine. Mmea huu una virutubisho vingi vinavyoweza kumsaidia binadamu kuboresha afya yake. Watu wengi wakifikia umri wa miaka 50 na kuendelea kumbukumbu zao kichwani huanza kupungua. Mmea huu ukitumiwa vizuri utaimarisha kumbukumbu zetu vizuri. Mmea huu hauishii hapo tu unatibu na magonjwa mengine kama kisukari huko India, China, Japan, Indonesia n.k hutumia sana. Magonjwa ya kuharisha damu kwa watoto katika hatua za mwanzo na matatizo ya tumbo kwa watoto. Matatizo ya tumbo kwa watoto huchanganywa na majani ya Fenugreek (Methi kwa kihindi). Ni mmea mzuri kwa mfumo wa neva (Nervous Disorders). Ni mmea mzuri kwa watu wenye matende (elephantiasis) juisi yake hupakwa sehemu zilizoathirika.
Pia ni mmea mzuri sana ukichanganywa  na mmea wa Trichodesma Indicum kutibu utasa kwa wanawake (Female Sterility) Hapa ni vizuri tukaelewana kuwa mwanamke asiwe na matatizo ya hedhi (Menstrual Pain) kutoka uchafu sehemu za siri (Usaha), uzito mkubwa sana n.k kama ana matatizo haya atibu kwanza. Pia hutibu magonjwa ya ngozi na vidonda vinavyotokana na kaswende. (Syphilitic Sores).
Pia majani yake huko India hutumika kutengeneza supu, Chatne, Chai, Juisi na kuchanganya kwenye chapati.
Tahadhari: Inashauriwa kutumia juisi kidogo ya mmea huu kwa sababu ina nguvu sana.
Kwa kuwa huu mmea unaweza kupanda kwenye bustani au kwenye makopo ya kupandia maua tunashauri kila familia ipande ili kuboresha afya.
Ukifanya jitihada za kututembelea ofisini utajua tunatibu maradhi mengine pia ikiwamo homa ya matumbo (Typhoid), Malaria, michirizi inayosababishwa na ujauzito( Stretch Marks in Pregnancy), mkanda wa Jeshi (Herper Zosters), Magonjwa ya ngozi, tumbo, kuimarisha kinga ya mwili, kuondoa gesi tumboni, kupunguza makali ya saratani, kisukari, BP ya kupanda. Mengine ni pamoja na maumivu makali wakati wa hedhi (Dysmenorrhea), kutoka damu nyingi wakati wa hedhi (Menorrhagia), kukawia kuingia hedhini (Amenorrhea), matatizo ya kukoma kwa hedhi (Menopause), kulegea kwa uzazi (vagina discharge), miguu kuwaka moto, vidonda vya tumbo, kufunga kuharisha, matatizo ya uvimbe wa kizazi na mengine mengi ambayo si ahisi kuyaorodhesha isipokuwa baadhi.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

MAAJABU YA KARAFUU (SYZYGIUM AROMATICUM) KUTIBU MAGONJWA MBALIMBALI


I



Karafuu ni tumba lililokauka la maua yasiyofunguka yanayopatikana kutoka mti mzuri wa kati na kijani. Mti huu una shina lilinyooka na hukua kufikia kimo cha mita 10 hadi 12.
Karafuu imekuwa ikitumiwa India na Uchina kwa zaidi ya kwa zaidi ya miaka 2000 kama kiungo cha kulinda kuoza meno na kutoa harufu mbaya yaaani pumzi mbaya.
Mti wa karafuu una asili ya visiwa vya Molluca. Wachina walipata kiungo hiki mnamo karne ya 3 K.K (Kabla ya Kuzaliwa Kristo).
Karafuu ziliingizwa Alexandria mapema mwaka 176 B.K (Baada ya Kuzaliwa Kristo). Mnamo karne ya 4 hivi B.K ulijulikana vema katika meditarrania na katika karne ya 8 ulaya nzima.
Inasemekana huko visiwa vya pemba na unguja (Zanzibar) karafuu ililetwa na sultani mmoja ikiwa imewekwa kwenye fimbo ya mwanzi leo hii Zanzibar ndio mzalishaji anayeongoza kwa kuzalisha karafuu nyingi ulimwenguni.
Sifa ilizonazo karafuu ni wanga (carbohydrates), Protini, mafuta (Volatile oil), nyuzinyuzi (crude fibre), jivu la hydrochloric acid, calcium, phosphorus, iron, sodium, Potassium, thiamine (Vit B1), Riboflavin (Vit B2), Niacin (Vitamin B3), vitamin A na C.
Mafuta hupatikana kwenye vitumba vya karafuu, kikonyo na majani.
Karafuu hutibu magonjwa mengi kama kutuliza maumivu ya meno, kutoa gesi tumboni, kuchafuliwa moyo, kuyeyusha chakula tumboni, kuimarisha viungo vya kiume (Sex Stimulant), kuimarisha mzunguko wa damu mwilini, kuzuia kutapika, kipindupindu, kikohozi, Asthma, Masikio, maumivu ya Misuli (Muscular Cramps), kuumwa kichwa, styes (an inflammation around the eyelash).
Matumizi mengine ya karafuu huchanganywa kwenye curry powder, pilipili, mdalasini, binzari na viungo vingine. Wahindi hutumia kuongeza ladha kwenye betel quid (pan pati). Mafuta ya Karafuu pia hutumika katika viwanda ya perfume, sabuni, ni kuongeza ladha kwenye madawa n.k
Tunashauri kila familia kuzingatia matumizi ya karafuu ili kulinda afya zetu.
Ukifanya jitihada za kututembelea ofisini utajua tunatibu maradhi mengine pia ikiwamo homa ya matumbo (Typhoid), Malaria, michirizi inayosababishwa na ujauzito( Stretch Marks in Pregnancy), mkanda wa Jeshi (Herper Zosters), Matatizo ya meno, Magonjwa ya ngozi, tumbo, kuimarisha kinga ya mwili, kuondoa gesi tumboni, kupunguza makali ya saratani, kisukari, BP ya kupanda. Mengine ni pamoja na maumivu makali wakati wa hedhi (Dysmenorrhea), kutoka damu nyingi wakati wa hedhi (Menorrhagia), kukawia kuingia hedhini (Amenorrhea), matatizo ya kukoma kwa hedhi (Menopause), kulegea kwa uzazi (vagina discharge), miguu kuwaka moto, vidonda vya tumbo, kufunga kuharisha, matatizo ya uvimbe wa kizazi na mengine mengi ambayo si rahisi kuyaorodhesha isipokuwa baadhi.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

ROSELLE (HIBISCUS SABDARIFFA)



.

Mmea wenye faida nyingi kwa binadamu

 Mmea huu asili yake ni nchi ya Sudan, sasa unapatikana katika maeneo yote ya tropiki. Bara la Asia unapatikana nchi za India, Korea, China n.k. Afrika magharibi unapatikana nchi za Mali, Burkina faso, Senegal na Ivory Coast na Afrika Kaskazini. Afrika mashariki kenya, Uganda na Tanzania. Katika Tanzania hulimwa katika mikoa ya Dodoma na Ruvuma, Mbeya ndio wameanza kuchangamkia kulima. Mkoani Dodoma hutumia maua yake kutengeneza juisi na pombe ya kienyeji (Choya) na mvinyo. Roselle hutumika kama chai ya kuburudisha na chai yake ina nguvu ya kuongeza mkojo na huleta kuongezeka kwa utoaji wa nyongo na jasho.
Roselle ina vitamin C, D, B-1, B-2, Chuma (Irion), Phosphorus, Calcium. Magnesium, Omega -3, Beta-Carotene na Amino Acid 18 zilizo muhimu kwa mwili wa binadamu kama lysine na agrinine.
Maua ya Roselle hutumika kuongeza damu (HB), kuimarisha mifupa( Prevents Osteoporosis), kuimarisha utendaji wa Ubongo ( antioxidant for brain), Kuimarisha afya ya ngozi (preserve the skin smooth and reduce wrinkles), kuimarisha utendaji wa utumbo (increased intestinal peristaltic), kupunguza shinikizo la damu( anti hypertension). Kuzuia magonjwa ya figo na moyo (inhibit kidney damage, diabetes, coronary heart diseases and growth of cancer for anti oxidant content is very high).
Majani hutumika kwa kikohozi, matatizo ya figo, kupunguza shinikizo la damu na kuimarisha utendaji wa utumbo. Mbegu zake nazo zina faida nyingi kiafya, mizizi na majani yake pia hutumika kutibu magamba ya miguuni (cracks in the feet), majipu na vidonda vilivyooza na kuvifanya vipone haraka pia ukitengeneza losheni ya majani hutibu vidonda.
Mizizi yake hutumika kuongeza hamu ya chakula. Katika majaribio ya Roselle ulionyesha tendo la kuchelewesha ukuaji wa bacteria za kifua kikuu, kwa hiyo kunywa chai hii mara kwa mara kwa tiba yoyote uliyopewa ya kifua kikuu.
Ni vema kila familia kupanda katika maeneo yetu ili kuboresha afya zetu.
Pia tunatibu Taifodi (Typhoid), Malaria, michirizi inayosababishwa na ujauzito( Stretch Marks in Pregnancy), mkanda wa Jeshi (Hyper Zosters), Magonjwa ya ngozi, tumbo, kuimarisha kinga ya mwili, kuondoa gesi tumboni, kupunguza makali ya saratani, kisukari, BP ya kupanda, Maumivu makali wakati wa hedhi (Dysmenorrhea), kutoka damu nyingi wakati wa hedhi (Menorrhagia), kukawia kuingia hedhini (Amenorrhea), matatizo ya kukoma kwa hedhi (Menopause), kulegea kwa uzazi (vagina discharge), miguu kuwaka moto, vidonda vya tumbo na kufunga kuharisha, matatizo ya uvimbe wa kizazi n.k
 

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com