Pages

Monday, September 5, 2022

MAJI: SEHEMU MUHIMU YA MLO WA BINADAMU

 

Kwanini tunahitaji maji mwilini.?

Je tunahitaji maji kiasi gani.?

Haya ni maswali ambayo kila binadamu anapaswa kujiuliza, kwasababu haina maana yeyote kama tunakunywa maji kila wakati,lakini tusijue faida yake mwilini.

Maji ni muhimu kwa makuzi na ulinzi wa miili yetu kwa kuwa yana kazi nyingi za mchakato wa kibaolojia mwilini.

Maji ni sehemu muhimu ya mlo wowote wa binadamu na hata  wanyama.Ndio maana mtu yeyote akishakula lazima atatafuta  maji ya kunywa. Katika mwili wa mtu mzima, asilimia kati ya 50 hadi 70 ya uzito wake ni majimaji, na bila maji muda wa uhai wa mwili unakuwa hatarini katika kipindi cha saa au siku chache.

Watu wengi hawanywi maji ya kutosha kwa siku, na matokeo yake ni kukaukiwa maji mwilini, na kusababisha madhara mengine kama ya kuumwa kichwa, uchovu na kushindwa kuwa makini.Mchakato wote wa lishe hauwezi kufantika vizuri bila ya maji. Maji ni muhimu sana mwilini kwani: Hurekebisha joto la mwili, Husaidia katika uyeyushaji wa chakula

Kukauka maji kwa muda mrefu mwilini kunaweza kuchangia matatizo kadhaa ya kiafya kama vile kutoenda haja kubwa na ugonjwa wa figo.

Je unahitaji maji kiasi gani.?

Kwanza ni muhimu kuanza kunywa maji angalau glasi moja tu mara unapoamka  asubuhi.

Pili jiwekee birika la maji mezani kwako, iwapo upo kazini, ili iwe rahisi kwako kunywa maji kila unapohitaji wakati wa kazi.

Kama upo katika mahangaiko wakati wote wa mchana, ni vyema ukabeba chupa ya maji, ili uweze kunywa maji wakati wote utakapojisikia kiu.

Ongeza kiwango chako cha ulaji matunda na mboga, kwani mboga na matunda yana kiwango kikubwa cha maji na faida nyingine kadhaa za kiafya.

Mwili wa binadamu na wanyama hupata maji yake kwa njia kuu tatu. Kwanza kunywa maji yenyewe kama kinywaji au kwakunywa viburudisho vingine kama vile soda. Maji pia yapo katika vyakula vigumu tunavyokula.

Yapo pia maji yanayotengenezwa katika mwili ikiwa ni matokeo ya mmeng’enyo wa kikemikali ndani ya mwili.

Mtu mzima kwa wastani anatakiwa kunywa angalau lita 2.5 za maji kwa siku, kati ya kiasi hiki, 1.8 lazima ipatikane kwenye vinywaji halisi, ikiwa na maana ya glasi 6 au 7 hivi kwa siku.

Unywaji huu unatakiwa kuongezwa wakati wa majira ya joto au baada ya kufanya kazi iliohitaji nguvu ili kurejesha uwiano wa maji katika mwili.kunywa maji yasiyochanganywa na chochote,bado ndio njia madhubuti ya kurejesha maji yanayopotea kutoka mwilini.

Maji ni mojawapo ya zawadi ya pekee ambayo mungu alitupatia. Karibia magonjwa yote yanayomsibu mwanadamu yanatibika kwa kuyatumia maji tu. Unapotumia Tiba ya maji unaepukana na kuumwa ugonjwa wa kichwa, presha, upungufu wa damu, kupooza, mapigo ya kasi ya moyo na kuzimia,kikohozi,pumu,kifua kikuu,kiungulia,kuharisha damu, bawasiri,kisukari,,matatizo ya macho,matatizo ya pua,masikio na koo.

Baada ya kuamka asubuhi mapema, kabla ya kupiga mswaki na kunawa uso, kunywa bilauri nne za maji, usile wala kunywa chochote mpaka dakika 45. Baada ya kunywa bilauri za maji ndipo upige mswaki na kunawa uso. Usinywe maji pale umalizapo kula chakula cha asubuhi, cha mchana  au cha usiku hadi baada ya saa moja au saa mbili zipite epuka kwenda kulala mara tu baada ya kumaliza kula chakula.

Kwa wagonjwa waliodhaifu inashauriwa waanze mpango huu kwa wakunywa bilauri moja au mbili na polepole waongeze idadi hata kufikia bilauri nne. Shinikizo la damu kunywa mwezi mmoja, matatizo ya gesi siku kumi, kufunga choo miezi sita, kisukari mwezi mmoja, kifua kikuu miezi mitatu, saratani miezi sita, Tumia maji salama kila wakati.

 

Thursday, August 11, 2022

PANDA MIMEA YA BAHATI NYUMBANI KWAKO

Miti na mimea ni zawadi bora kwa binadamu na hutoa chakula , hewa safi, makazi na mahitaji yote ya maisha.Ni manufaa sana kuwa na mimea karibu nasi  kama iwezekanavyo . Kwasababu hiyo ,bustani ya ndani ni kuwa moyo .Inasaidia katika kutunza nyumba ya kijani na safi , mimea ya ndani pia huwa na manufaa mengi ya afya .Baadhi ya mimea ya ndani au mimea bustani ni kufanyika kumfikisha bahati na mafanikio katika nyumba. Mimea hii inasemekana kung’ara nishati chanya popote kukua . Orodha ya mimea michache unaweza kupanda katika nyumba yako kuleta furaha na bahati ni kama ifuatavyo.

Kurimbasi(Basil) huleta upendo ,shauku,mali,bahati na uzuri wa nyumba yako,na tunaweza wote kutumia kidogo.Kurimbasi unaweza kuitumia kwa radha ya chakula chako . Na pia inajulikana kwa kuwa dawa ya mfadhaiko , antiseptic na antibacteria pia.

Rosemary kuongezeka ubongo wako nguvu , unaweza kukusaidia kupata kupumzika usiku mzuri . Mimea hii huvutia upendo na moyo tamaa , inatabia ya ulinzi na utakaso , husaidia na uponyaji , na unaweza hata kutumia katika mapepo .

Mimea aina ya miniature roses ina nguvu kubwa ya viumbe hai wote . Huvutia upendo , uponyaji na bahati , kutoa ulinzi na uponyaji na kusaidia na uganga wa kila aina .

Roses maua meupe husaidia kusafishwa na uponyaji na nguvu chanya . Roses nyeupe na nyekundu husaidia ibada na uchu. Roses rangi ya peach husaidia amani, kiroho na urafiki . Roses rangi ya pink husaidia kimapenzi upendo , utamu , furaha na kucheza . Roses aina fuchsia husaidia tamaa kwa maisha , asili kujitegemea upendo , upendo wa kina na kukubalika ya mwili yako ya kimwili.

Roses rangi ya lavender husaidia kiroho. Roses rangi nyekundu husaidia uchu, kina na upendo wa kweli. Ndio maana biashara ya maua ya roses ni kubwa huko ulaya na Asia.

Jasmine huvutia upendo wa fedha katika nyumba yako, na moyo ndoto unabii. Jasmine mafuta inajulikana kwa kuwa  moja wa kuamsha tamaa ya kiume au kike nguvu zaidi, hivyo hii ni mimea ya ajabu kwa watoto wachanga moja au mtu kutaka kuweka mahaba hai. Maua jasmine mara nyingi huvaliwa na makuhani juu. Cha ajabu maua jasmine hufungua maua usiku, ambayo kwa mawazo yangu inawafanya hata baridi.

 Limao na ndimu pamoja na kuwa mkali na furaha limao na ndimu ni kitu ya ajabu  kwa kuwa karibu na nyumba. Ni mfano wa utakaso na urafiki. Panda karibu na nyumba yako.

 

 

 

 

 

 

Sage ni maalum kwa ajili ya sifa yake ya ulinzi, pia inawakilisha kutokufa, maisha marefu, hekima na utoaji wa matakwa. Panda nyumbani kwako mimea ya sage.

 kwa leo naishia hapa tutaendelea wiki ijayo

Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

 


Mazingira Natural Products

Mbeya

Simu; +255 754 807401, +255 719 564276

Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com

Blogu: mazingiranp.blogspot.com

 

NSEBHE MTI UNAOTIBU MAGONJWA MENGI.

 


NSEBHE ni mti unaotibu magonjwa.NSEBHE hupatikana katika mikoa ya Mbeya, Rukwa, Morogoro, Tabora, Arusha, Mikoa ya Pwani na Kagera(Rulangaranga) nk. Jina la kibotania huitwa Erythrina Abyssinica. Wanyakyusa huita NSEBHE. Wasafwa huita Lisebhe.

Mti huu sitauelezea sana ila naomba watanzania wote na wale wenye mapenzi mema na mimea, tuupande, tuutunze na kuulinda mti huu kwa sababu hutibu magonjwa mengi sana, Majani hutibu vidonda vya tumbo, kuharisha, vidonda na maumivu ya viungo kwa kuweka kwenye vidonda na kuchua kwenye viungo, kutapisha, kwa wanyama hutibu magonjwa ya ngozi. Maua yakitwangwa hutibu kuhara kwa damu, magome yakirostiwa na kutwangwa kuwa unga yanatibu vidonda vya kuungua, vidonda vinavyotoa usaha na uvimbe. Rojo linalotokana na vishina vya kijani vya mti huu hutibu ugonjwa wa Conjunctivitis unaosababishwa na Chlamydia trachomatis(trachoma).

Magome hutibu Malaria, magonjwa ya zinaa kama kaswende,kisonono, Amiba, kikohozi, kuumwa na nyoka, maumivu ya Ini, maumivu ya tumbo, kusokotwa na tumbo na surua(measles). Maua yakitwangwa hutibu maumivu ya sikio, mizizi hutibu vidonda vya tumbo,malaria, epilepsy, kichocho na blennorrhagia.

Wavuvi hutumia magome yake kama maboya ya kuvulia samaki, pia sisi zamani magome yake tulikuwa tunatumia kutengenezea mihuri kwa matumizi mbalimbali.Mti huu hutumika kutengeneza vinyago, stuli, ngoma, mizinga ya nyuki na bidhaa za mikono. Mbegu zake hutumika kutengeneza urembo wa shanga za kuvaa shingoni.

 

Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

 


Mazingira Natural Products

Mbeya

Simu; +255 754 807401, +255 719 564276

Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com

Blogu: mazingiranp.blogspot.com

 

SALADI HUONDOA SUMU MWILINI

 

 


Kilimo cha saladi ni moja ya kilimo cha mbogamboga aina ya kabichi ambacho wengi hawajui na hawakithamini hii ni tofauti na mataifa yaliyoendelea, ambao wao hutumia muda mwingi kufikiri namna ya kutunza afya zao.

Wakati huu twaweza kujiuliza kuwa ni wangapi wenye uwezo wa kupanda saladi na tukaitumia kuboresha afya zetu hapa Tanzania.

Jibu ni wachache sana, lakini nisizunguke sana labda nikukaribishe katika kilimo cha pekee ambacho hakina magonjwa mengi nacho ni kilimo cha saladi.

Jina la kibotania huitwa Lactuca Sativa. Waingereza huita Lettuce.

Saladi ziko aina nyeupe, kijani, nyeusi na nyekundu. Saladi ya kijani na nyekundu ndio zenye virutubisho bora.

Aina za saladi Romaine, Crisphead (Ice berg), Butterhead (Boston na Bibb) na Nyekundu na Kijani. Saladi zina vitamin A kwa wingi, Protini, Calcium, Vitamini C, Chuma, Vitamini K, Omega – 3 Fatty acids, Folate na potassium.

Saladi ikiliwa mara kwa mara husaidia kupunguza uzito, moyo kufanya kazi vizuri, kuondoa uwezekano wa kupata lehemu  ( Cholesterol). Wanaokosa usingizi watumie saladi, huondoa sumu mwilini, husaidia macho kuona vizuri, husaidia ngozi ya mwili kuwa na mwonekano mzuri, Huondoa anxiety, Husaidia uwezekano wa kutopata saratani ya damu na matiti na husaidia ubongo kufanya kazi yake vizuri na kuepuka ugonjwa wa Alzheimer’s.

Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

 


Mazingira Natural Products

Mbeya

Simu; +255 754 807401, +255 719 564276

Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com

Blogu: mazingiranp.blogspot.com

 

MUHOGO ZAO LA KARNE YA 21

 


            Leo nimekuandalia zao la muhogo .Na asili ya zao la muhogo ni Amerika ya kusini hasa brazil. Muhogo ni zao lenye  kustahimili hali mbaya kama ukame na mvua zisizoaminika,kutoa mazao mengi kwa eneo na  kustahimili mashambulizi ya magonjwa na wadudu.Jina la kibotania huitwa manihot esculenta au manihot utilisima.majina mengine huitwa manioc ,yucca root.waingereza huita cassava. zao la muhogo ni muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini.kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula  kikuu ambacho kinachukua 75%  ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya lindi na mtwara .kwa siku za karibuni muhogo unaongoza kwa kuongezeka katika umaarufu  kuliko mazao yote ya chakula nchini .Majani ya muhogo yana protini,vitamin B12,B-2,Beta Carotene na niacin, Iysine, Isoleucine, leucine, valine.Muhogo ukiliwa huzuia saratani na kutibu Arthritis,Conjunctivitis,kuharisha,flu,maumivu ya kichwa(headaches),kuongeza nguvu mwilini,kulinda na kurekebisha tishu za mwili ,kupunguza lehemu mwilini,kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo,kujenga mifupa na meno kuwa na nguvu(imara),kutunza metabolism kuwa ya kawaida, inasaidia kurekebisha moyo utende kazi yake vizuri na blood pressure(BP) na wale wenye heart rhythm wanashauriwa kula mihogo mara kwa mara kwa kuwa una potassium kwa wingi,huzuia kukosa choo na kupunguza uzito,huimarisha uzazi(enhanced fertility) na ndio maana watu wengi siku hizi wanakula mihogo mibichi, wale walio na tatizo la celiac watumie mihogo mara kwa mara mihogo haina Gluten,wenye kisukari wale mihogo kwa kuwa inapunguza kiwango cha sukari,huzuia saratani,huimarisha Probiotics na kuongeza kinga ya mwili, inazuia Neural damage in brain na kuzuia Alzheimer kwa matatizo haya tumia majani machanga ya muhogo kwa kuwa yana vitamin kwa wingi ,huzuia anemia na kusaidia damu kubeba oksijeni vizuri na husaidia kupunguza msongo na fadhaa.

         Majani ya muhogo muhogo wenyewe yana kiwango kikubwa cha sumu aina ya hydrocyanic acid amabayo ni hatari kwa mwili lakini vitu hivyo vikipikwa sumu hiyo huondoka na kuwa salama kwa mtumiaji.      

  Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.

 


Mazingira Natural Products

Mbeya

Simu; +255 754 807401, +255 719 564276

Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com

Blogu: mazingiranp.blogspot.com