Pages

Thursday, August 31, 2017

MAAJABU YA KARANGA PORI KUTIBU MAGONJWA MBALIMBALI



 Zao la karanga pori ni miongoni mwa zao lisilopewa kipaumbele sana hapa Tanzania, zamani wakati wa ujana wangu, bibi mzaa mama alipanda miti miwili, ilikuwa inakuwa na karanga nyingi tulikuwa tunakula bila kujua faida yake kwa mwili wa binadamu.
Mama mkwe wangu Tamali Mwasomola amepanda miti mitatu na ukifika msimu wa karanga watoto huja kununua.
Miaka ya hivi karibuni kampuni ya maparachichi Rungwe na Enterprise works walikuwa wakihamasisha wananchi wa mkoa wa Mbeya kupanda karanga pori zinazoanza kuzaa kwa muda mfupi tofauti na zingine.
Asili ya karanga pori ni Australia. Pia nchi zingine zinazolima kwa wingi ni Brazil, Indonesia, Kenya, New Zealand na Afrika kusini. Karanga pori ya Hawaii ina ladha nzuri, kuna aina saba ya karanga pori, lakini zinazoliwa ni aina mbili.
Ø  Majina ya kibotania huitwa Macadamia Integrifolia na  Macadamia Tetraphylla, waingereza huita Macadamia Majina mengine huitwa Australia nut, Queen sland nut na Bush nut.
 . Nchini Kenya wanaita Njugu ya macadamia. Hapa Tanzania hustawi sehemu za Rungwe, Ifakara, Morogoro, Kilolo, Arusha, Hai na Lushoto nk.
Karanga pori ina vitamin A, Protini, Chuma, Thiamin, rifboflavin, niacin,folates, zinki, shaba, calcium,phosphorus,potassium na magnesium. Karanga pori ina kizuia Oxidants kama polyphenols, Amino acids, flavones na selenium. Pia kuna sucrose, fructose, glucose na maltose nk.
Faida zitokanazo na kula mara  kwa mara karanga pori ni kukinga magonjwa ya moyo (Heart Disease) kwa kuondoa lehemu, kupunguza uzito, kuimarisha afya ya mifupa, inaboresha akili ukichanganya na maziwa pia zabibu. Ina nyuzi lishe inayosaidia umeng’enyaji wa chakula tumboni na kuondoa ukosefu wa kwenda haja kubwa kwa shida, ina mafuta ya Oleic acid yanayohamasisha kuwa na kumbukumbu nzuri.
Hufanya seli na tishu za mwili ziwe na nguvu, Hupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo, saratani na arthritis kwa kuwa kuna omega – 3 na Omega – 6 fatty acids, kuondoa radiko huru (free radicals) ambayo husababisha magonjwa ya saratani ya matiti, kizazi na saratani ya Tezi dume. Huchelewesha ngozi kuzeeka haraka, Huzuia ugonjwa wa trans- epidermal water loss (TEWL), Hulinda ngozi na nywele zisiharibirike haraka, Huzuia kukatika ovyo kwa nywele zisiharibike haraka, inasaidia kuboresha afya kwa wale waishio na VVU na Ukimwi hasa kwa kuongeza kinga ya mwili na karanga pori, hutumika kutengenezea mafuta ya kula, kuongeza ladha kwenye chokoleti, ice cream, keki, sherbets, maandazi, brittles, candies, mafuta ya kupaka mwili na mafuta ya nywele.
Pia karanga pori huliwa zikiwa mbichi, kavu au kuchoma kwenye moto.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.
 

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com



8 comments:

  1. Nesphory L. Katunzi (0754 533335)March 16, 2020 at 3:08 AM

    Mimi nimevutiwa sananakilimohiki na nipo tayari kupewaushauri ili nianze kulima sasa.

    Nitaendelea kuwasiliana nanyi kuweza kujua kuhusu hatua zote ninazotakiwa kufuata kuanzia kuandaa shamba hadikulitunza likiwalimepandwa.

    ReplyDelete
  2. Hellow. Samahani mimi nilikuwa naomba kuomba kuuuliza. Soko lake kwa Tanzania lipite na zinauzwa kwa kwa kiasi gani. Asante

    ReplyDelete
  3. Hellow. Samahani mimi nilikuwa naomba kuomba kuuuliza. Soko lake kwa Tanzania lipite na zinauzwa kwa kwa kiasi gani. Asante

    ReplyDelete
  4. Kama nauhitaji wa hizo karanga pori kwa matumizi binafsi naweza pata nipo dar itakuwa shilingi ngapi?

    ReplyDelete
  5. Na hii karanga pori ambayo unakula punje moja baada ya hapo unaanza kuharisha kwa maana ya kusafisha tumbo, hii ni ipi? Naomba somo

    ReplyDelete
  6. Mbona nsikia ukila karanga poring unaharisha?

    ReplyDelete
  7. Nilikula kilichonipata sintarudia tena...ukinywa tulia kwako unaeza endesha week

    ReplyDelete
  8. Mbeguzinapatkkanawapi?

    ReplyDelete