Pages

Friday, September 6, 2013

Maajabu ya Mmea wa Rumex (Sorrel)



)
Maajabu ya Mmea wa Rumex (Sorrel) Usambarensis katika kutibu mkanda wa Jeshi Msemwasemwa (Kinyakyusa), Kchambo (Wapare. Rumex (Sorrel) Usambarensis- Botanic ni mimea inayoota kwa mtindo wa vichaka vichaka inayopatikana katika mikoa ya Mbeya, Rukwa, Njombe, Ruvuma, Iringa na Kilimanjaro n.k mmea huu umeonekana kuwa na faida kubwa sana kwa afya ya binadamu na wanyama, kwa vile hutibu maradhi mbalimbali.
Tafiti mbalimbali zilizowahi kufanyika nchini Tanzania na Kenya  zinaonyesha umuhimu wa mmea huu kutibu magonjwa mbalimbali kwa mfano majani hutibu kikohozi na maumivu ya tumbo.
Mizizi yake na vikonyo vichanga hutumika kutibu kikohozi cha kawaida na Nimonia(Pneumonia), vidonda na majipu.
Pia mizizi yake ikitumiwa na mimea mingine ni dawa ya baadhi ya minyoo inayosumbua sana watu. Pia wazee wa zamani wal;itumia mmea mzima kwa kutibu ndui (Small Pox) kwa kuwaogesha wagonjwa.
Mazingira Natural Products ya Mbeya tumefanya utafiti wa mmea huu ukichanganywa na mimea mingine kama Black Nightshade n.k hutibu vizuri sana mkanda wa Jeshi (Herper Zoster’s) wa aina zote. Na ukitumiwa vizuri huimarisha kinga ya mwili kwa mtumiaji.
Lakini mmea huu hauishii hapo kwa wale wafugaji wa kuku hapa Mbeya wale wanaotumia watakubali bila shaka  yoyote ile kuwa mmea huu unafaa sana kuwalisha kuku hasa wale wanaotaga mayai hufanya kiini kuwa cha njano sana na kupunguza matatizo ya kuku  kudonoana ovyo.
Hili ni muhimu kwa mwananchi yeyote wa Tanzaniania kulifanyia kazi kwa kupanda na kutumia katika mazingira yake.
Imeandaliwa na Mtafiti Dr. Edgar Kajolo Kapagi
Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; 0754 807401, 0719  564276
Barua pepe: mnp.kaka@gmail.com

No comments:

Post a Comment