Pages

Saturday, April 28, 2018

MAFUTA YA MAWESE HUZUIA UWEZEKANO WA KUPATA SARATANI MBALIMBALI




Mafuta ya mawese hutokana na mmea wa mchikichi. Mchikichi huzalisha mafuta ya kupikia, dawa mbalimbali, diseli na mise. Mti wa mchikichi huweza kukua kufikia kimo cha meta 30. Matunda ni madogo yakiwa na shingo, Jumla mti mmoja unatoa kilo 50 za matunda.
Asili ya mchikichi ni Afrika magharibi ukanda wa Guinea.
Siku hizi michikichi inakuzwa zaidi Amerika na hasa Asia ya kusini, Malaysia na Indonesia.
Nchi Asilia za michikichi, kitropiki ya Afrika kanda ya Guinea, DR Congo, Benin, Nigeria, Senegal, Sierra leone na Togo. Afrika mashariki inapatikana Kenya, Tanzania na Uganda. Kuna aina mbili ya michikichi, Elaeis guineensis inayolimwa Afrika na Asia kusini. Elaeis oleifera inalimwa Amerika, michikichi ni zao mojawapo ya mazao ya mafuta ambalo hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kigoma, Mbeya na Tanga. Aidha zao hili hulimwa pia kwa kiasi kidogo katika mikoa ya Kagera, Pwani, Rukwa, Morogoro na Visiwa vya Pemba na Unguja. Kigoma ikiwa ni eneo muhimu kwa uzalishaji, huzalisha zaidi ya tani 2,000 za mawese na zaidi ya Tani 450 za mafuta ya mise.
Wasomaji wenzangu wa makala hii, mawese ninayoyaeleza ni yale yenye uhalisia wa rangi nyekundu na chungwa na si vinginevyo.
Kwenye mafuta ya mawese kuna vitamin A, D, E (Tocopherols) na Beta – Carotene kwa wingi. Mafuta ya mawese huongeza nguvu mwilini, huimarisha uwezo wa kuona, watu warika zote tuyatumie kwani wengi tuna matatizo ya macho kutokuona vizuri, huzuia uwezekano wa kupata Cardiovascular, Hupunguza uwezekano wa kupata saratani aina mbalimbali kwa kuwa yana Vitamini E kwa wingi, huimarisha Hormonal balance, huzuia upungufu wa vitamin kwa wakina mama wanaonyonyesha na watoto, huzuia uwezekano wa kupata magonjwa ya Alzheimes, huimarisha afya kwa wajawazito, kuimarisha kinga ya mwili na kuzuia kuzeeka haraka
TAHADHARI
Watu ambao wana lehemu mwilini (Had cholesterol) wasitumie mafuta ya mawese.
Carotenoids (Alpha, beta na gamma – carotenes)
Sterols (Sitosterol, stigmasterol na campesterol)
Vitamini E (tocopherols na tocotrienols)


Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi.
 

Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com

No comments:

Post a Comment