Pages

Wednesday, April 6, 2016

PILIPILI RAFIKI WA MOYO WA BINADAMU

Pilipili hulimwa sehemu nyingi ulimwenguni. Pilipili ziko za aina nyingi ulimwenguni kama Pilipili Kichaa, Pilipili Mbuzi, Paprika, capsicum, Bell pepper, Capsicum Frutescens na cayenne pepper nk. Kwa leo nitaelezea pilipili ya cayenne pepper.
Jina la kibotania huitwa Capsicum Anuum, Waingereza huita cayenne pepper.
Cayenne peppers ina vitamini A,B,C,E,  Betacarotene, Chuma, Phosphorus, Calcium, Thiamine, Riboflavin na Niacin nk.
Pilipili aina hii wengi hutumia kama kiungo katika mapishi yao mbalimbali. Pilipili ina kimeng’enyo aina ya Capsaicin ambacho kina manufaa makubwa kwa mwili wa binadamu.
Watu wa mashariki ya mbali kama India,Thailand nk hutumia sana pilipili katika vyakula vyao na ni mara chache sana hushambuliwa na matatizo ya moyo. Pilipili hii ikitumika vizuri huzuia kushambuliwa kwa Moyo na kufanya usipate na HBP na hupunguza uwezekano wa kupata kiharusi. Pilipili hutibu vidonda vya tumbo japo watu wengi huona kama inaleta vidonda vya tumbo. Inapotumiwa na wenye vidonda vya tumbo mwanzoni tumbo huuma sana lakini kadri unavyoendelea kutumia tumbo huacha kuuma. Pilipili hutibu maummivu ya viungo    (baridi ya yabisi) rheumatism, kuteguka, maumivu ya misuri, kuvimba kwa viungo (arthritis) maumivu ya kiuno, na kuuma kwa mshipa wa nyuma ya paja. Twanga kijiko kimoja kikubwa cha pilipili mbichi au kavu na kijiko kimoja kikubwa cha mafuta ya mawese. Mchue mgonjwa kwa mchanganyiko huu kwa nguvu sana hadi asikie maumivu.Na uendelee kuviweka viungo katika hali ya joto. Tumbo kujaa hewa na bawasiri ongeza pilipili katika chakula chako. Kisukari cha miguu tumia kama maumivu ya viungo , lakini tibu miguu kwa uangalifu isichubue ngozi. Magonjwa ya ngozi na mkanda wa jeshi (herpers zoster) hutumia mafuta ya mawese yaliochanganywa na pilipili kwa kiasi ambacho mgonjwa atakuwa bado anauwezo wa kuvumilia maumivu.
Pilipili hutibu Arteriosclerosis, Asthma, Bronchitis, Mafusa, Kikohozi, kutosagika vizuri kwa chakula, Homa ya manjano, Bandama, Figo, Pancreas, Flu, na Varicose veins.
Tumia kijiko cha chai cha pilipili weka kwenye kikombe cha maji yaliyochemka. Kunywa nusu kikombe mara tatu kwa siku mpaka mgonjwa apone.
Kutibu vidonda weka unga wa pilipili juu ya vidonda
Pilipili hutumika kutengeneza sosi ya pilipili nk.

Pia tunatoa ushauri, mafuta kwa waliopooza na wanobabuka na jua kama Albino (Herbal sunscreen oil) na Tiba. 
Mazingira Natural Products
Simu: +225 754 807401-0719 564 276
Barua pepe:mnp.kaka@gmail.com
Blogu:mazingiranp.blogspot.com

No comments:

Post a Comment