Pages

Wednesday, April 6, 2016

MIUJIZA YA MATANGO

Matango ni mboga inayopendwa   sana na kulimwa kwa wingi ulimwenguni. Na hutumiwa sana wakati  wa joto la kiangazi kwa kupooza mwili kutokana na joto na kuondoa kiu ya maji. Kuna aina ya matango American slicer,European cucumber na Gherkins nk. Jina la jumla la kibotania huitwa  cucumis sativus. Waingereza huita cucumber. Na asili ya matango ni India na huita kheera/sukasa na yalikuja kujulikana misri, Ugiriki, Roma na China miaka mingi iliyopita. Sasa hivi yameenea kote ulimwenguni. Yanalimwa kwa wingi  India, Pakistani, china, America na nchi nyingine nyingi. Tanzania pia tunalima na kuyatumia.
Matango yana vitamini B,C,K,Calcium, Phosphorus,Chuma,Shaba,Potassium,Sodium,Manganese,Magnesium,Sulphur,Silicon,Chloline na Fluorine nk.
Kula matango mara kwa mara husaidia kulinda ubongo kuwa na afya njema, kuzuia uwezekano wa kupata saratani kwa kuwa matango yana polyphenols inayoitwa lignans inayopunguza uwezekano wa kupata saratani ya matiti, Uterine,Ovarian na tezi dume. Matango yanapigana na muwako wa mwili (unaowasha au kuchoma). Matango yanazuia Oxidant, matango hudhibiti msongo wa mawazo kwa kuwa yana vitamini B1, B5 na B7 (biotin) Zinazopunguza mtu kuwa na wasiwasi na kuzuia nguvu ya kipigo cha msongo wa mawazo. Matango  yakiliwa hufanya moyo uwe na afya njema kwa kuwa yana potassium inayopunguza shinikizo la damu. Matango yanasaidia umeng’enywaji wa chakula vizuri tumboni.Vidonda vya tumbo na majipu. Ukiumwa na mdudu kata slesi ya tango na bandika penye tatizo. Huongeza utokaji wa mkojo na kufanya bandama liwe na afya njema, Tumbo na utumbo mkubwa kuwa na afya njema. Matango yanapoliwa husafisha damu na kuzuia magonjwa ya ngozi. Matango yakiliwa na ganda lake huzuia mawe ya kwenye figo. Yanaondoa uric asidi katika mwili unapoyala matango. Matango yanaondoa au kuzuia magonjwa ya Ini,Figo na Koo. Wenye kisukari na kupunguza uzito wa mwili watumie matango kuwa sehemu ya mlo wao. Matango husimamisha kichefuchefu na kutapika. Matango husaidia kipindupindu unatengeneza glasi moja la juisi ya tango na unachanganya na maji ya nazi(dafu) unakunywa kila baada ya saa moja inaleta matokeo mazuri kwa mtumiaji. Inaondoa baridi yabisi (Rheumatism) kuvimba miguu kwa kuchanganya na juisi ya karoti na Beetroot. Hutumiwa kuleta uzuri wa ngozi sugulia uso na kipande cha tango.Osha uso na juisi (maji yake utaona matokeo mazuri baada ya wiki moja). Pia matango hutengeneza saladi kwa kuchanganya na Karoti, Nyanya, Radishi, Kabeji na maziwa ya mgando.
                  ANGALIZO
Vitamini na madini mengi yapo kwenye Ngozi kwa hiyo unapotumia usitoe maganda ingawa mengine ni machungu kidogo ikiliwa na maganda lakini bado hufaa zaidi.
Pia matango aina ya American Slicer na European cucumber hufaa kwa tiba na saladi.
Matango aina ya Gherkins hufaa kwa tiba na Achali.

No comments:

Post a Comment