Pages

Friday, May 18, 2018

BAMIA HUSAIDIA KWA WANAO WAHI KUFIKA KILELENI MAPEMA



 Nianze kwa kumshukuru mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi kwa kuendelea kunipa afya njema pamoja na wewe msomaji wa Gazeti hili. Hakika ni jambo la pekee ambalo Mungu ametutunuku kwa maana wapo hospitalini wakitafuta huduma kwa ajili ya afya zao. Bamia ni mboga iliyotokea kupendwa miongoni mwa wa watanzania wengi pengine kwa kutotambua au kutambua umuhimu wake kwa afya ya binadamu.
Bamia hulimwa katika nchi za Tropiki na nusu Tropiki. Jina Bamia limetokana na jina Bamya asili yake nchi ya waThai (Thailand)
Nasisi watanzania tunaita BAMIA. Jina la kibotania huitwa Abelmoschus esculents au hibiscus esculents linn. Waingereza huita Okra au lady fingers.Bamia ina wanga , mafuta , protini, sodium, folate , calcium, magnesium,Vitamini A na C. Bamia ikiliwa mara kwa mara hupunguza sukari kwenye damu kwa wagonjwa wa KISUKARI. Bamia ikilo wekwa usiku kucha kwenye maji na kunywewa  hupunguza lehemu (cholesterol) na kuweka sawa sukari mwilini. Bamia ikipondwa na kuwa rojo inafaa kupaka vidonda vya kuungua na matatizo ya ngozi . Bamia ina MUCIN inayolinda matatizo mengi yanayotokea ndani ya tumbo na utumbo kwa hiyo ikiliwa utakuwa na afya njema kila wakati. Mtokoso wa bamia ambazo hazija komaa sana hutibu maumivu ya mucous membrane inayosababisha matatizo ya upumuaji. Juisi ya Bamia hutibu maumivu ya koo yanayo sababishwa na kikohozi. Mtokoso wa majani, matunda yake hutibu mfumo wa ukojoaji kwa wanaume na wanawake kama maumivu ya mkojo unapokojoa, Kaswende na kisonono. Majani na mizizi ikipondwa na kupakwa vidonda hupona haraka. Juisi ya bamia hutibu homa , kuharisha na maumivu ya tumbo . Juisi ya bamia hutibu muwasho wa ngozi na ni“moisturizer” ya ngozi. Bamia zikiliwa mara kwa mara zinasaidia kwa wale wanaowahi kufika kileleni wakati  watendo la ndoa. Bamia zikiliwa mara kwa mara huima risha na kuboresha kumbukumbu nakuufanya uti wa mgongo ufanye  kazi yake vizuri . Mbegu za bamia zikikaangwa nakusagwa hutumika kama chai na kuongeza utokaji wa jasho. Mbegu za bamia hutibu mwako wa misuli. Mtokoso wa bamia hutibu kichwa na Arthritis. Bamia zina nyuzinyuzi kwa wingi na maji zinafaa sana kwa wale wenye tatizo la kuto pata choo vizuri na gesi ya tumboni kutoka vizuri kwa njia ya kinyesi . Bamia ni kilainishi kizuri cha tumbo zitumiwe mara kwa mara. Bamia zinalainisha ngozi zinafanya usipate chunusi nk. Tumia bamia ambazo hazija komaa sana na zilizo chumwa ndani ya siku tatu zaidi ya hapo usitumie.
Pia tunatoa ushauri, mafuta kwa waliopoza na Tiba.
Mazingira Natural Products
S.L.P 1338 Mbeya
Mob:+255719564276-0754807401
Email:mnp,kaka@gmail.com     
Blogu:maziniranp.blogspot.com

No comments:

Post a Comment