Pages

Saturday, May 26, 2018

KULA KABEJI YA ZAMBARAU NA MNAVU UEPUKANE NA VIDONDA VYA TUMBO


Je nitajuaje kama nina Vidonda vya Tumbo?
Dalili za ugonjwa wa tumbo,
i)kuchoka choka sana bila sababu maalum, Mgongo kuuma, kiuno, kupungukiwa au kupoteza kabisa nguvu za kijinsia,
Kizunguzungu, kukosa usingizi  au kulala mara kwa mara .  Maumivu makali chini ya kifua  kwa ndani kama kwamba  unachomwa na kitu chenye ncha kali , maumivu hayo wakati mwingine  mgongoni ambapo huchoma kama sindano yenye sumu na kuacha maumivu makali  wengi huita chembe chembe ya moyo. Dalili zingine kichefu chefu, kiungulia, tumbo kuwaka moto, maumivu makali sehemu kilichopo kidonda,  kukosa choo na kupata choo kigumu na chenye kukatika katika kama choo cha mbuzi, shida ya moyo,  kutapika nyongo, kutapika damu au kuharisha, sehemu za mwili kupata ganzi hasa  miguu na mikono. Dalili nyingine ni kukosa hamu ya kula, kula kupita kawaida, kusahausahau na hasira. Kwa kweli ni vigumu kueleza maelezo yote apatayo mgonjwa wa vidonda vya tumbo hasa kwa mgonjwa  aliye sugu kwani hakuna hata kiungo kimoja mwilini atakachokwambia ni kizima.
Vipimo vya vidonda vya tumbo.
ii)Njia iliyo sahihi na nzuri zaidi ni kupima kwa daktari kipimo kiitwacho barium meal x-ray, Endoscopy au H.Pylori test.
Ulaji wa kabeji na kutengeneza juisi yake utakuepusha kupata vidonda vya tumbo. Pia unapokula mboga ya mnavu wasafwa  huita sungwe utaepukana na kupata vidonda vya tumbo wasafwa hula mboga za kabeji na mnavu mara kwa mara wengi wao hawana matatizo ya vidonda vya tumbo.

No comments:

Post a Comment