Pages

Saturday, May 26, 2018

FAIDA YA NDIZI


 Ndizi ni zao moja kati ya mazao ya matunda ambayo huzallishwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Kigoma, Tanga, Kagera na Mara. Jina la Kibotania linaitwa Musa paradisiaca na Kingereza huitwa banana.  Wandali huita Indunye na Wanyakyusa huita Amabifu /Amatoki, zao hili hutumika kama zao la chakula na tunda pia. Kando ya kula kama chakula tu, kuna malighafi nyingine tele katika mmea huu inayoweza kuufaidisha mwili wa binadamu kama tiba kwa magonjwa mbalimbali. Asili au tabia ya mmea huu inanukia, imetulia, kizuia vidonda, kiongeza mkojo na ni  kiamshi. Ndizi  ina vitamin, Virutubisho vya kuleta nguvu pamoja na aina nyingi za lishe muhimu. Pia ina madini ya chuma, potassium, Calcium, Sodium, Magnesium, Shaba, Manganese, Phosphorus, Sulphur, Silica, na Chlorine nk. Ndizi husaidia katika kuboresha hali za watu kwa maana zina kemikali za serotonin “na” dopamine” ambazo humfanya mtu kujisikia vizuri.  Ndizi hutibu athari zinazotokana na pombe kwa kusawazisha Msukumo wa damu (kwa msaada wa potassium) pamoja na kuzuia kiungulia. Maua ya ndizi  hupunguza utokaji wa damu nyingi wakati wa hedhi kwa kuyaponda ponda na kunywa.  Maua huuchemshwa na kuliwa na wenye kisukari. Pia utomvcu wake ni dawa ya kutia sikio linalouma. Ndizi mbivu ikipondwa na kuchanganywa na maziwa, sukari ni nzuri kwa kukuza watoto. Ndizi mbivu ikichanganywa na ukwaju na chumvi kidogo ni tiba nzuri kwa hatua za mwanzo za kuharisha na kuharisha damu. Wale wanaosumbuliwa na usagaji wa chakula ni vizuri watumie ndizi na kikombe kimoja cha maziwa wakati wanaenda kulala. Wale wenye bawasiri waponde ndizi na kuzichemsha pamoja na maziwa kikombe kimoja na watumie mara tatu kutwa. Hutibu kikohozi kwa kuchanganya na pilipili manga kidogo na kula mara tatu kutwa. Wenye   kifua kikuu waponde ndizi na kuchanganya na nusu kikombe cha maziwa ya mgando yaliyo salama, kijiko cha chai cha asali na kikombe kimoja cha maji ya dafu (nazi) na kutum,ia mara mbili kwa siku. Homa ya manjano na homa ya matumbo waponde ndizi na kuchanganya na kijiko cha chakula cha asali wale mara mbili kutwa kwa siku kadhaa. Majivu ya maganda ya ndizi ni tiba nzuri kwa vidonda. Ndizi mbichi unga wake ni lishe nzuri kwa wenye kisukari na wale wenye kuvuja damu wenye shida usagaji wa chakula, na wenye asidi tumboni. Majani mabichi hutumika kutibu macho yanayouma na kutuliza maumivu ya kichwa pia ponda majani na kuweka juu ya kidonda. Majivu ya shina la mmea ni tiba nzuri kwa wenye  vidonda. Juisi ni nzuri kwa wenye shida  ya mishipa ya fahamu, kuharisha, kuharisha damu na manjano. Pia inazuia damu isitoke katika vidonda vya kujikata nk. Mizizi ni tiba nzuri kwa maumivu ya ngozi laini ya njia ya mkojo na ya uzazi/uke. Mizizi iliyochujwa na kuongeza asali ni tiba ya kubanwa kwa ini na mlinzi mzuri wa ini. Utumiaji wa ndizi mbivu mara kwa mara huondoa tatizo la kufunga choo, udhaifu wa mwili na vidonda vya tumbo. Pia ukila ndizi mbili zina kutosha kukupatia nguvu za kufanya kazi ngumu kwa muda wa dakika tisini. Ndizi hutumika kwa matumizi mbalimbali kama Ugali, Chips nk.

MAZINGIRA NATURAL PRODUCTS
MBEYA
Simu: +225 754 807 401 +255 719 564 276
Barua pepe: mnp.kaka@gmail.com
Blogu: mazingiranp.blogspot.com 

No comments:

Post a Comment